BOMOABOMOA KUZIKUMBA NYUMBA 4000 KATIKA BONDE LA MSIMBAZI


Mkuu wa Kitengo cha Sheria Balaza la Taifa la usimamizi wa mazingira Tanzania (NEMC), Manchale Heche akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam juu ya zoezi la Bomoabomoa maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi nakuwataka wananchi waliojenga katika fukwe za bahari Kingo za mito na mikondo ya bahari kuhamisha mali zao mapema. 

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Manispaa za jiji la Dar es salaam zitafanya zoezi la kuondoa wavamizi maeneo yote ya Mabondeni, kingo za mito  na za Bahari, maeneo ya wazi, maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi zaidi ya 150 katika  jiji la Dar es salaam. Bomoa bomoa ya leo inaendelea katika Bonde la mto msimbazi.
                                           
                                          
Wakati bomoabomoa hiyo ikiendelea kuna bomoabomoa inaendelea kupisha treni ya mwendokasi na barabara pia wananchi ambao wamepata matatizo hayo wanalani vikali bomoabomoa hiyo na kusema serikali imetumia nguvu wakati kesi zao zipo mahakamani kuweka pingamizi,
Wananchi wanasema serikali inachukua nguvu kubwa sana katika bomoabomoa hiyo na kufanya watu kuishi kwa shida nyingi kwani wengi wao walijenga nyumba kwa kutumia mikopo.
                                          Gari la Bomoabomoa katika maeneo ya msimbazi


                                          Watu wakitoa vitu kabla ya kubomolewa

Maoni