KATIBU WA CHADEMA MKOA WA NJOMBE AMESEMA UWEZO WA MSUKUMA NI MDOGO SANA

Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Njombe Alatanga Nyagawa ambaye pia ni wakili ameweza kueleza kitendo ambacho kimechukuliwa na Raisi wa mawakili nchini Mh Tundu Lissu ni kitendo chema cha kukemea vikali juu ya kulipuliwa kwa jengo la wanasheria hapa nchini,


Nashangaa kuona watu wengine wanasema mgomo huo upo kisiasa na kuwaskia wanasiasa eti Mbunge wa geita kulichukulia kisiasa wakati ni swala la hatari sana bila kukemea vikali kuna matendo zaidi ya haya yanaweza kuendelea kutokea hapa nchini na ikawa ni hatari sana leo watu mmesahau matukio ambayo yametokea hapo nyuma uvamizi katika vituo vya radio na utekaji sehemu mbalimbali na sasa mmesahau ila huu ni mwendelezo wa hayo matukio,

Nashangaa kuona MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI,JAJI MKUU NA WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA Kuwa kimya katika tukio hili ambalo ni hatari sana hapa nchini na wao ni wanasheria pia tuseme wajaweza kuguswa ata kidogo kuhusu tukio hili na kumwachia Mbunge wa geita kusema baada ya serikali ambaye uwelewa wake wa sheria na mambo mbalimbali ni mdogo sana na kubaki na ushabiki wa kichama,

Msukuma atambui mambo kwahiyo mimi naona kama anachekesha kwani awezi kubishana na Lissu maana uwelewa wake kwa Lissu ni mdogo sana kisheria na kutetea taifa hili la Tanzania na kusema serikali ya tanzania ikiendelea kupuuza vitu vya msingi ambavyo vinasimamiwa ndani ya nchi hii nchi hii tunaipeleka pabaya sana ingawa kwasasa tutashindwa kujua ila tukifika huku ndipo tutabaki na majito mjukuu,

Haya matukio usipoweza kupinga leo tambua kesho yataweza kukukuta wewe na sijui utakimbilia wapi?

Alimaliza na kusema watanzania tunatakiwa kuungana bila hivyo tutalipeleka taifa letu pabaya sana.

Maoni