TANGAZO KWA WAOMBAJI KAZI WALIOITWA KWENYE USAILI WA TRA

Waombaji kazi waliotwa kwenye usaili wa kada mbalimbali za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanasisitizwa kuwa hakuna utaratibu wa kuomba kubadilishiwa kituo cha kufanyia usaili ambacho mwombaji kazi amepangiwa.
Usaili huo ambao utafanyika katika Vituo kumi hapa nchini, vimepangwa kwa kuzingatia anuani za waombaji ambazo waliainisha kwenye barua zao za maombi ya kazi, hivyo mgawanyo wa vituo vya kufanyia usaili huo umezingatia ukaribu wa Mikoa kwa kila kanda ili kuwaepushia usumbufu wasailiwa kusafiri umbali mrefu.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano,

Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma.

Maoni