Wakimbizi Tanzania wapunguziwa mgao wa chakula tatizo kubwa ni pesa

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limesema limepunguza mgao wa chakula cha misaada kwa wakimbizi 320,000 wanaoishi kaskazini magharibi mwa Tanzania kutokana na uhaba wa fedha kutoka kwa wafadhili. Katika taarifa iliyoitoa leo, WFP imesema inahitaji kwa dharura kiasi cha dola milioni 23.6 kuweza kukidhi mahitaji ya chakula cha wakimbizi hadi mwezi Desemba. Wakimbizi hao ni kutoka Burundi na CongoMwakilishi wa WFP nchini Tanzania Michael Dunford amesema mgao wa chakula utazidi kupunguzwa iwapo wafadhili hawatatoa misaada mara moja. Umoja wa Mataifa umekuwa pia ukiwaomba wafadhili kuwasaidia zaidi ya wakimbizi milioni mbili wa Sudan Kusini walioko katika nchi jirani.


Maoni