MH KIKWETE BORA TUPOTEZE MAJIMBO MATANO YA CCM ILA LA MH LISSU TUCHUKUE KAULI YA 2010.

Kumbukumbu ya serikali ya awamu ya nne chini ya Mh Jakaya kikwete aliweza kutambua uwezo mkubwa wa Mh Lissu katika uchambuzi wa sheria mbalimbali mpaka kuogopwa na serikali na serikali iliweza kuwa makini katika kuwasilisha miswada mbalimbali bungeni maana walikuwa wanatambua uwezo mkubwa wa Lissu

Mh Kikwete Rais mstaafu aliweza kusema katika uchaguzi wa 2010 kwa bora tukose majimbo matano ila jimbo la Lissu tufanye Lolote tuweze kulichukua

Yote ni kutokana na uwezo wake wa kuisimamia serikali ya Tanzania ndani ya bunge na nje ya bunge mpaka Kikwete kuona Lissu ni kikwazo kikubwa ila akuweza kupigwa risasi au kufanyiwa uvamizi wowote ule au kufatiliwa na gari lolote lile ambalo aliweza kusema liliweza kumfatilia,
Mh Kikwete  aliweza kutambua uwezo wake mkubwa katika sheria

Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Raisi Magufuli toka ameweza kuingia katika madaraka Mh Lissu amekuwa akikamatwa na kupewa kesi zaidi  ya 12 za uchochezi yote ni kukosoa serikali ya magufuli kabla ajapigwa na risasi 38,

Utaweza kutambua Lissu mapambano yake sio ya jana wa juzi ni mda mrefu amekuwa katika mapambano juu ya Taifa hili la Tanzania.

Maoni