YANGA YASUBIRI KIPIGO AMBACHO WALIKIPATA AZAM KUTOKA KWA NJOMBE MJI MKOANI NJOMBE SIKU YA JUMATANO

Wadau wa Timu ya Njombe Mji jana waliweza kukutana katika ukumbi wa Turbo Njombe mjini kuweza mikakati ya kuweza  pointi tatu katika mechi ya kesho kutwa jumatano katika uwanja wa sabasaba njombe mjini,
Kikao cha wadau wa Njombe Mji kiliweza kuongozwa na mwenyekiti wa club ya Njombe Mji na wajumbe wa club pamoja na kamati ya ufundi ili kuweza kujua jinsi gani?wataweza kuchukua pointi tatu,
Mwenyekiti wa club amesema timu ipo viziri kwasasa na tusahau mechi ya kwanza zidi ya prison ambayo iliweza kufungwa 2 kwa 1 ila ni kutokana na mikakati ilikuwa ijakamilika na wachezaji wao wengine walikuwa wajakamilisha usajili wao pia ambao kuna wanigeria na mnyarwanda
Mwenyekiti ameweza kueleza timu ipo vizuri ila ijaweza kupata mzamini wa kudumu kama wenzao singida united na club nyingine ingawa tumetuma proposal sehemu mbalimbali mpaka sasa tujapata majibu kwahiyo tunajibana hivyohivyo kutokana na hari yetu ambayo tunayo na
Mwenyekiti aliweza kusema tunatakiwa kujipanga katika kushangilia timu yetu ingawa ninajua hapa kuna wanayanga wengi na wanasimba kwahiyo uyanga tuweke pembeni na kuweza kuweka uzalendo wa timu yetu katika kushangilia pasipo kukata tama,
Mwenyekiti ameweza kuwaimiza mashabiki wa mpira na wapenzi wa njombe mji kuweza kufika mapema sana uwanjani ili kuweza kusaidia katika kushangilia na kupanga mikakati ya ushangiliaji kwani tupo nyumbani tunatakiwa kuonyesha tupo nyumbani ili kuweza kuwapoteza nguvu hawa wapinzani wetu,
Pia Wadau wa njombe mji waliweza kuchangia pesa juu ya Club yao kuweza kufanikisha mipango mbalimbali ambayo ni faida kwa club yao kwenye mambo mbalimbali ya Club
Wadau wa Njombe Mji pia waliweza kutoa maoni mbalimbali juu ya kuboresha club yao iweze kukaa sawa na kuweza kufanya makubwa katika ligi kuu ya Tanzania na kuchukua nafasi nzuri katika msimamo wa ligi hapo mbeleni ingawa ndio mara ya kwanza kuingia maana miaka mingi imepita toka Nazareti kutoka katika ligi kuu Tanzania
Pia Benchi la ufundi limeweza kusema limekaa poa na yanga kutoka katika uwanja wa sabasaba labda waje uwanjani peku ndipo wanaweza kushinda na kusema hapa sio Dar Hapa Njombe lazima wapewe salamu zao ili wawapelekee wazalamo.





Maoni