IGP SIRRO ATAKIWA KUJIBU MASWALI YA MH JOHN HECHE JUU KUJADILI SHAMBULIO LA MH LISSU.



IGP Sirro huna mamlaka na huwezi kunyamazisha Watanzania kujadili shambulio la kinyama alilofanyiwa Lissu,
Lissu ni kiongozi wa Watanzania ambae ameshambuliwa vibaya, Watanzania wana haki ya kuhoji:
1.nini kinaendelea kuhusu uchunguzi wa jambo hili na nani mpaka sasa wamekamatwa.
2.kwanini kumekuwepo kusitasita na kujivuta kwa serikali na Bunge kwenye matibabu ya Lissu wakati ni haki yake.
3.kwanini zinakuwepo taarifa za kujichanganya kwa viongozi wa serikali kuhusu jambo hili.
4.kwanini mnatumia nguvu nyingi sana kuzuia watu kujadili jambo hili!!
5.kwanini mnazuia hata watu kukusanyika kumuombea mh Lissu?....
6.kwanini serikali inakataa usaidizi wa kiuchunguzi kutoka kwenye vyombo vingine vyenye uwezo na nyezo za kisasa zaidi kwenye jambo hili?!
Kwa kifupi watu wataendelea kujadali na kufuatilia,Lissu sio mnyama kwamba afanyiwe jaribio baya la kuondoa uhai wake alafu watu wanyamaze, 
IGP Sirro acha kufanya siasa tekeleza wajibu wako kwenye suala hili tunakata kujua nani walifanya tukio hilo.

Maoni

Chapisha Maoni