Upinzani waahirisha maandamano dhidi ya tume ya uchaguzi Kenya


Muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa) umefutilia mbali maandamano ambayo yalikuwa yamepangiwa kufanyika nchini humo leo kushinikiza mageuzi katika tume ya uchaguzi.
Muungano huo, kupitia taarifa, umesema umechukua hatua hiyo kupata fursa ya kuomboleza watu ambao wameuawa kwenye maandamano ya awali.
Nasa, muungano unaoongozwa na waziri mkuu wa zamani Raila Odinga, ulikuwa umeahidi kufanya maandamano kila siku kushinikiza mageuzi katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa marudio.
Taarifa iliyotumwa na msemaji wa Bw Odinga, Dennis Onyango, imesema maandamano hayo yatarejelewa tena Jumatano.


Uchaguzi mkuu umepangiwa kufanyika tarehe 26 Oktoba baada ya Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya uchaguzi wa tarehe 8 Agosti na kuagiza uchaguzi mpya wa urais ufanyike katika kipindi cha siku 60.
"Hii ni hatua ya muda ya kuuwezesha muungano huu kuwazuru na wafuasi wake waliokumbana na ukatili wa polisi na jamaa za waliojeruhiwa au kuuawa," taarifa hiyo ilisema.
Jumatatu, kijana wa miaka 18 aliuawa kwa kupigwa risasi wakati wa maandamano kati ya polisi na wafuasi wa upinzani mjini Kisumu.


Waliouawa maandamano ya baada ya uchaguzi Kenya 33

Watu ambao Amnesty na HRW wanasema waliuawa na polisi Nairobi
  • 67 Idadi ya watu ambao mashirika hayo mawili yanakadiria waliuawa kote nchini Kenya
  • 9 Umri wa Stephanie Moraa Nyarangi aliyepigwa risasi Mathare
AFP/Getty
Mtoto wa miaka miwili pia alijeruhiwa begani baada ya kupigwa risasi wakati wa maandamano hayo.
Mashirika mawili ya kutetea haki za kibinadamu ya Amnesty International na Human Rights Watch jana yalisema watu 67 wameuawa tangu kuanza kwa maandamano ya upinzani baada ya uchaguzi.

SOURCE BBC 

Maoni