HABARI KUTOKA KENYA:RAIS KENYATTA NDIO MSHINDI WA UCHAGUZI MKUU KENYA KUTOKA KWA JAJI MARAGA.

 

Jaji Maraga amesema majaji kwa kauli moja wameamua kwamba kesi zote mbili hazina msingi.

Kesi ya Bw Harun Mwau na wanaharakati wawili Njonjo Mue na Khelef Khalif zimetupiliwa mbali.

Uchaguzi wa 26 Oktoba umedumishwa, sawa na ushindi wa Bw Kenyatta. Kila upande utasimamia gharama yake..

 

Maraga: Kesi ya pili ilihusu utaratibu na uhalali wa uchaguzi

Mgombea akijiondoa kabla ya uchaguzi, matokeo yake ni gani? Kuna mgombea aliyejiondoa kikamilifu?
IEBC na mwenyekiti wake waliandaa uchaguzi kwa kufuata Katiba na sheria za uchaguzi?
Uchaguzi wa 26 Oktoba ulitimiza viwango vya katiba vya uchaguzi huru na wa haki?
Matokeo ya kutofanyika uchaguzi maeneo mengine kunaathiri uchaguzi?
Uchaguzi uliathiriwa na visa vya udanganyifu?
Marekebisho ya sheria yaliyoidhinishwa Oktoba yanaathiri chochote, yalifuata sheria?

    Mambo muhimu yatakayoangaziwa na majaji

    Katika Kesi majaji watatakiwa kutoa uamuzi kuhusu masuala yafuatayo:
    • Iwapo tume huru ya taifa ya chaguzi na mipaka (IEBC ) ilifaa kuteuwa upya wagombea urais au la.
    • Uamuzi pia utatolewa na mahakama hiyo juu zaidi juu ya ya ikiwa kujiondoa kwenye uchaguzi huo kwa mgombea wa upinzani Raila Odinga.
    • Majaji pia watatoa uamuzi kuhusu ikiwa baada ya tume ya IEBC kushindwa kuendesha uchaguzi katika ameneo bunge 25 kati ya 290 kunahalalisha ama kubatilisha matokeo ya uchaguzi.
    • Aidha Mahakama hiyo itawaeleza waKenya ikiwa tume ya uchaguzi (IEBC) ilikuwa na uwezo wa kuandaa uchaguzi wa haki na huru baada ya kugubikwa na mgawanyiko miongoni mwa wajumbe wake.
    • Kwa upande mwingine Wakenya watasubiri kusikia uamuzi wa mahakama kuhusu kama ghasia zilizotokea kabla na baada ya uchaguzi wa marudio wa urais ziliathiri ama hazikuathiri matokeo ya uchaguzi na kuufanya kuwa usio wa haki na huru au la.
    • Mahakama itatoa ufafanuzi juu ya dosari ya karatasi za kupigia kura, maarufu kama form 34A ziliathiri matokeo ya uchaguzi.
    • Hukumu hii inasubiriwa kwa shauku kubwa na raia wa Kenya pamoja na kwingineko duniani, huku wengio wakijiuliza hatma ya Kenya.

Maoni