POLISI WAPIGA MABOMU NA KUSIMAMISHA MSAFARA WA NAIBU KATIBU MKUU MNYIKA VITU VIMEPOTEA SIMU ,PESA NA VINGINE.

Picha ya Patrick Ole Sosopi











 

Naibu Katibu Mkuu CHADEMA - Bara *Mhe. John J. Mnyika* leo Novemba 19, 2017 ameongea na wakazi wa Momba katika mkutano wa kumnadi Mgombea Udiwani kupitia CHADEMA katika uchaguzi wa marudio katika Kata hiyo ya Ndalambo iliyopo wilaya ya Momba mkoani Songwe.

Mkutano huo ambao ulishirikisha Viongozi mbalimbali wa CHADEMA wakiwemo Wabunge Mhe. Ernest Silinde - Mbunge wa Momba, Mhe. Frank Mwakajoka - Mbunge wa Tunduma na Mhe. Risala Kabongo - Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Songwe ulimalizika kwa polisi kuzuia msafara wa Viongozi hao na kuanza kupiga mabomu ya machozi ovyo.

*Updates kuhusu mabomu yaliyorushwa kwenye msafara wa Mnyika na gari lake lililochukuliwa na Polisi...*

Baada ya Polisi kupiga mabomu msafara huo na baada ya kumpiga dereva wa Naibu Katibu Mkuu huyo wa CHADEMA walitoa vitu vyake kwenye gari zikiwemo nyaraka mbalimbali na mabegi na kisha kuondoka na gari lake jambo lililolazimu Mhe. Mnyika pamoja na Viongozi wengine kuelekea Kituo cha Polisi Tunduma kwa ajili ya kufuatilia suala hilo ambapo mpaka sasa gari limeshakabidhiwa kwa Viongozi hao wa CHADEMA lakini Mhe. Mnyika ajaona simu zake mbili ambazo zimepotea pia kufuatia tukio hilo kuna upotevu wa Shilingi laki nane (800,000/=) za Kitanzania pia Dereva wa Naibu Katibu Mkuu John Mnyika aliyetoweka baada ya kuwakimbia Polisi waliokuwa wakimdhibiti tayari ameshajitokeza.

Taarifa zaidi tutazidi kuwaletea...

Habari CHADEMA
Kanda ya Nyasa


Maoni