Ofisa mtendaji mkuu wa kampuni ya Acacia, Brad Gordon
***
Ofisa mtendaji mkuu wa kampuni ya
Acacia, Brad Gordon na ofisa mkuu wa fedha Andrew Wray wamejiuzulu,
kampuni hiyo ya uchimbaji wa madini imetangaza.
Kampuni hiyo yenye migodi mitatu ya
dhahabu kaskazini magharibi mwa Tanzania imetangaza kuwa wawili hao
wataondoka rasmi Acacia mwishoni mwa mwaka huu. Hata hivyo, taarifa
inayopatikana kwenye tovuti ya kampuni imeeleza kuwa, Peter Geleta
ataiongoza kampuni hiyo katika kipindi cha mpito huku Jaco Maritz
akiongoza kitengo cha fedha.
Maoni
Chapisha Maoni